Romans 16:1-6
Salamu Kwa Watu Binafsi
1 aNapenda kumtambulisha kwenu dada yetu Foibe, mtumishi katika kanisa la Kenkrea. 2 bNaomba mpokeeni katika Bwana ipasavyo watakatifu na kumpa msaada wowote atakaohitaji kutoka kwenu, kwa maana yeye amekuwa msaada kwa watu wengi, mimi nikiwa miongoni mwao. 3 cWasalimuni Prisila ▼▼ Prisila kwa Kiyunani ni Priska, hivyo tafsiri nyingine zimemuita Priska.
na Akila, watumishi wenzangu katika Al-Masihi Isa. 4Wao walihatarisha maisha yao kwa ajili yangu; wala si mimi tu ninayewashukuru bali pia makanisa yote ya watu wa Mataifa. 5 eLisalimuni pia kanisa linalokutana nyumbani mwao.
Msalimuni rafiki yangu mpendwa Epaineto, aliyekuwa mtu wa kwanza kumwamini Al-Masihi huko Asia.
6Msalimuni Maria, aliyefanya kazi kwa bidii kwa ajili yenu.
Copyright information for
SwhKC